Duration 1:15

Hazina ya COVID-19 kwa ushirikiano na Wakfu wa Equity zatoa vifaa vya kujikinga na corona

708 watched
0
2
Published 24 Jul 2020

Hazina ya dharura ya COVID-19 kwa ushirikiano wa wakfu wa Equity zinaendelea kusambaza vifaa maalum vya kuwakinga wahudumu wa afya na maambukizi ya virusi vya Corona. Katika kaunti ya Wajir, shughuli hiyo iliongozwa na meneja mkuu wa benki ya Equity Francis Adel alisema kuwa hospitali 68 humu nchini zitanufaika na mpango huu. Mhudumu mmoja wa afya amefariki leo Wajir baada ya kuugua kwa siku mbili. Maafisa wa afya wamedokeza kuwa sampuli tayari zimetumwa hapa Nairobi kubaini iwapo marehemu alikua na ugonjwa huo. Kaunti za Bomet, Homa Bay na Trans Nzoia pia zimesambaziwa vifaa hivyo leo.

Category

Show more

Comments - 0